Tuesday, July 20, 2021

SWALI NA JIBU: Mabadiliko ya fasihi ya Kiswahili na Jamii

 SWALI:  Fasihi ya Kiswahili imekuwa ikibadilika sambamba na mabadiliko ya jamii husika .Jadili kauli hiyo kwa mifano maridhawa kutoka katika riwaya ya Kiswahili

   Fasihi imejadiliwa katika mitazamo mbalimbali mfano ule unaodai kuwa fasihi “literature” ni jumla ya maandishi yote katika lugha Fulani,( Wallek na Warren 1986:20).Mtazamo mwingine ni ule unaodai kuwa “literature” au fasihi ni maandishi bora au jamii ya kisanaa yenye manufaa ya kudumu (H. Summers 1989:357). Pia mtazamo uliozuka hapa Afrika Mashariki na kuenea zaidi miaka ya 1970 ni ule unaosema kuwa “Fasihi ni hisi ambao unafafanua kwa njia ya lugha (Ramadhani J.A 2:6)”.Hivyo kwa ujumla Fasihi ni utanzu au tawi la sanaa ambalo hutumia lugha hutumia lugha ya mazungumzo au ya maandishi ili kufikisha ujumbe kwa hadhira husika.

Fasihi ya Kiswahili,pia imejadiliwa na wataalamu mbalimbali,mfano (Syambo na Mazrui 1992), anjadili fasihi ya Kiswahili kuwa, ni ile inayoandikwa kwa kiswhili tu,iwapo inazungumzia utamaduni wa Kiswahili au utamaduni mwingineo maadamu fasihi hiyo imetumia lugha ya Kiswahili na imefuata mbinu za ufasaha wa lugha hiyo. Mabadiliko, ni hali ya kutoka hatua moja kenda nyingine ,mabadiliko hayo yanaweza kuwa chanya au hasi. Fasihi ni zao la jamii hivyo haina budi kubadilika kulingana na jamii.Riwaya kama kazi moja ya fasihi ni hadithi ndefu ya kubuni yenye visa vingi, wahusika zaidi ya mmoja yenye maelezo na mazungumzo yanayozingatia kwa undani na kwa upana zaidi.Ni kweli kwamba fasihi ya Kiswahili imekuwa ikibadilika sambamba na mabadiliko ya jamii,mabadiliko hayo yako katika vipindi mbalimbali kama ifuatavyo;

   Kipndi kabla ya uhuru, Hiki ni kipindi ambacho jamii iliishi chini ya utawala wa wakoloni ambapo watu walinyanyaswa, walikosa kukosa haki, walikandamizwa kutokana na utawala wa mabavu wa wakoloni.Katika kipindi hiki kuliandikwa riwaya maarufu inayoitwa “Uhuru wa watumwa” ambayo iliandikwa na “James Mbotela” (1934) ambayo ilikuwa ni zao la mashindano yaliyoendeshwa na kamati ya Kiswahili ya Afrika mashariki mwaka 1930 na kuwa riwaya ya kwanza ya Kiswahili ,riwaya hii iliandikwa kuonyesha ushenzi uliokuwa ukifanywa na Waarabu, Waswahili, na Waislamu ambao walikuwa wakiendesha biashara ya utumwa na kuwachora , kuwakweza waingereza kwa kuwaona kama wakombozi walioletwa na Mungu kukemea ukandamizaji huo.Hivyo riwaya hii iliandikwa kutokubaliana na utumwa , uovu, au uonevu uliokuwa ukifanywa na waarabu.

   Kipindi baada ya uhuru, Hiki ni kipindi ambacho jamii iliishi kwa kutaka uhuru wa kweli  ambapo wananchi walitegemea uhuru wa kweli na ujenzi wa jamii mpya na ukombozi, ambapo viongozi baada ya uhuru baadhi walikuwa wakiendeleza kasumba za ukoloni kwa kutowajali wananchi ambapo jamii ilijaa manyanyaso, matabaka , ukandamizaji na ubadhilifu wa mali za umma. Hivyo riwaya nyingi zilitungwa kusuta usaliti huo uliofanywa na viongozi wa kiafrika ili kuweza kujenga jamii mpya yenye usawa , haki na uhuru. Katika kipindi hiki riwaya za “Shaaban Robert” ziliandikwa kusuta usaliti huo mfano wa riwaya ni Siku ya watenzi wote  kilichoandikwa na “Shaaban Robert” mwaka (1960-62), riwaya hii iliandikwa kusuta usaliti uliofanywa na viongozi kwa raia wao.Riwaya hii inasadifu kabisa mabadiliko katika kipindi hicho, kwani ni kweli viongozi waliwasaliti wananchi wake.

   Kipindi cha azimio la Arusha,Hiki ni kipindi ambacho ilikusudiwa kujenga misingi ya ujamaa na kujitegemea, Katika kipindi hiki kuliibuka ujamaa uliolenga umoja na mshikamano, haki na usawa pia, vijiji vya ujamaa vilianzishwa ili kuhimiza mshikamano huo. Ziiliandikwa riwaya zilizokuwa zikihimiza umoja na mshikamano mfano wa riwaya iliyokuwa inalenga kuhimiza huo ilikuwa “Mtu ni utu” kilichoandikw na( Mhina G, 1971). Hivyo mabadiliko ya jamii katika kipindi hiki yalisababisha pia kuibuka kwa dhamira ya ujenzi wa jamii mpya ili kuhimiza mabadiliko hayo.

   Kipindi baada ya ujamaa, Baada ya ujamaa kuliibuka mabadiliko yaliyosababisha kuanguka kwa ujamaa ambayo yalienda sambamba na anguko la uchumi, ambapo jamii ya wakati huu ilianza kuishi maisha magumu tofauti na matarajio yao yaliyolengwa na azimio la Arusha, watu walikata tamaa,walipoteza matumaini.Hvyo riwaya zikaandikwa kueleza anguko hilo kwa kushindwa kukidhi matarajio yaliyolengwa ,ziliandikwa riwaya zinazoonyesha kuwa zinausuta mfumo huo wa ujanaa.Mfano wa riwaya ni “Kaptula la Marx” kilichoandikwa na “Euphrase Kezilabahi” ambapo kiliongelea kuwa viongozi waliiga mfumo ambao hawakuwa na uwezo wa kuutekeleza na ndio maana Kezilahabi akaandika na kusema “Mtazunguka wee lakini mtarudi palepale” hii ilikuwa ni kusuta kuwa hawakuwa na uwezo wa kuendana na mfumo huo. Vilevilie kitabu kingine kilichoandikwa na Euphrase Kezilahabi kinaitwa “Nyota ya huzuni” ambacho kiliandikwa kuonyesha kufifia kwa matumaini, yaani yale waliyolenga kuyafikia katika kipindi hicho cha ujamaa yalionekana kutofanikiwa.Vitabu hivi viliandikwa kwa mafumbo sana ili kukwepa rungu la tabaka tawala ,mfano kitabu chake Euphrase Kezilahabi cha “Kaptula la marx”.Hivyo Fsihi ya wakati huu ilienda sambamba kabisa na mabadiliko ya jamii.

   Kipindi cha vita ya kagera,Hiki ni kipindi a,mbapo jamii ilikuwa katika vita ambapo watu wengi walijawa na hofu kubwa kutokana na vita hiyo ,ambapo watu walipoteza mali, maisha na kulikuwa na kuwabeba vijana katika vita ambapo walipigana ili kutetea taifa la Tanzania.Riwaya ziliandikwa kuhimiza vijana waeze kujikaza na kuwa jasiri katika katika kupambana na hali hiyo ya vita .Kukaandikwa riwaya kama  Mashujaa wakaza kamba”(1978) riwaya iliyoandikwa na P.Shija”Vita hivi vya Uganda na Tanzania  viliibua waandishi walioandilka riwaya zilizolenga  kuwatia moyo, na kuwapa hamasa au kuwahamasisha vijana hao, pia kulenga kusisitiza ukakamavu,wawapo vitani . Hivyo asihi ya wakati ilisadifu maisha halisia ya kipindi hiki.

   Kipindi cha utandawazi, Hiki ni kipindi ambacho kimetawaliwa na maendeleo ya sayansi na teknolojia, ambapo katika kipindi hiki kulizuka soko huria, ambapo jamii ya kipindoi hiki ilianza kuishi kwa kuiga mambo mbalimbali kutoka katika mataifa ya kimagharibi , kukatokea mambo mengi ambayo yanahusisha kutafuta mali kwa nguvu, kizazi au jamii iliyojaa na tamaa, umasikini ulliokithiri, umalaya na mitandao ya kijamii iliyochangia kuharibu maadili ya watu .Katika kipindi hiki kumeibuka dhamira za riwaya zinazolenga kueleza mambo mazito ya kijamii, kama vile mauaji ya albino, kutokana na dhana potofu walizonazo watu wa kipindi hiki.Kutokana na ukatili huo ziliibuka riwaza ya  Takadini” iliyoandikwa na Ben Hanson ,pia kuna masuala ya mapenzi yanayopelekea watu kupoteza kazi,pia mapenzi yanapunguza ufanisi katika kazi, mfano riwaya ya “Mfadhili” iliyoandikwa na “Hussein Tuwa” (2004), na kitabu kinachoongelea masuala ya umasikini “Usiku utakapokwisha” kilichoandikwa na “Mbunda Msokile”(1990)  na masuala ya tamaa, ambapo watu wa jamii ya kipindi hiki wametawaliwa na tamaa zinazowapelekea kuingia katika matatizo makubwa, mfano riwaya ya “Kiroba cheusi” kilichoandikwa na “Laura Pettie” (2019), ambaye anwatumia wahusika Morena na Fatumata kueleza suala la tamaa na matatizo ya tamaa.Hivyo kutokana na mabadiliko ya jamii riwaya nayo imekuwa ikibadilika vivyo hivyo.

   Hivyo basi fasihi na jamii ni vitu viwili ambavyo ni kama baba na mtoto haviwezi kutenganishwa ,kwa kuwa fasihi inachipukia kutoka katika jamii na mabadiliko hayo ya kijamii ndio mwongozo au chanzo cha fasihi mpya.Na jamii sio mgando bali ina mabadilika badilika kutokana na vipindi tofauti ambavyo vinaikumba jamii hiyo, na fasihi nayo inafuata mabadiliko hayo

 

 

MAREJELEO

Mulokozi M. M, (2017). Utangulizi wa fasihi ya Kiswahili;Muccoi Printing Press:Dar-es-salaam

Msokile, M.(1990). Usiku utakapokwisha.Dar es salaam University Press: Dar-es-salaam

Kezilahabi, E. (1999).Kaptula la Marx.Dar es salaam University Press: Dar-es-salaam

Pettie L, (2019);Kiroba cheusi;Mfuko wa riwaya ya waridi:Dar-es-salaam

 

No comments:

Featured Post

 SOMA SIMULIZI ZENYE KUSISIMUA HAPA A. UTAJIRI WENYE UCHUNGU     UTAJIRI WENYE UCHUNGU-1     UTAJIRI WENYE UCHUNGU-2      UTAJIRI WENYE UCH...