Tuesday, July 20, 2021

SWALI NA JIBU: Hatua kuntu za kupima uhalali wa mtihani




1. (a). Tathimini mtihani wa kidato cha nne mwaka 2018.Kisha onesha uhalali na kuaminika   kwake

     


MPANGO KAZI

UTANGULIZI

·         Maana ya mtihani

·         Maana ya tathmini

KIINI

·         Ubora na udhaifu wa mtihani wa kuhitimu kidato cha nne (2018).

HITIMISHO

MAREJELEO


     Mtihani,ni njia ambayo mtu hupimwa kutokana na alichokisoma au alichofundishwa ili atambuliwe kwamba alielewa au hakuelewa. Ni njia rasmi zaidi ya kupima mafanikio katika mchakato wa kufundisha na kujifunza baada ya kipindi maalaumu kumalizika.Tathimini,ni utaratibu wa kupima na kuchunguza hali halisi kwa lengo la kupata data zitakazomwezesha mwalimu au mtahini kufanya maamuzi yanayohusu urekebishaji au uboreshaji wa mambo mbalimbali katika elimu. Hivyo mchakato wa tathimini  huchambua ,hukusanya  na kuzipa daraja la ubora taarifa za ufundishaji na ujifunzaji  ili kuamua ni kwa kiasi gani malengo yaliyoainishwa kwenye mtaala yamefanikiwa. Ifuatayo ni tathimini ya mtihani wa Taifa wa Kiswahili kidato cha nne (2018).Kwa kuanza na ubora wake;

      Maelezo yaliyotolewa katika kila sehemu ya mtihani yapo wazi, uwazi wa maelezo unamsaidia mwanafunzi kuyaelewa na kuyajibu vyema maswali yanavyotakiwa kujibiwa, pia katika maelezo ya jumla ya mtihani mfano, “sehemu “B” (Alama 25) Sarufi na Utumizi wa lugha”, jibu maswali yote katika sehemu hii, uwazi huu humsaidia mwanafunzi kujua sehemu husika inahitaji nini, na mada husika ya maswali hayo.

     Maswali yanaendana na kiwango cha elimu cha watahiniwa, katika mtihani huu wa kidato cha nne (2018 ), maswali  yaliyomo  yametolewa  kwa kuzingatia mada za kiwango cha elimu ya Tanzania kwa ngazi ya elimu ya sekondari, pia mada zimechukuliwa kama muhtasari ulivyo ainisha mada hizo,mfano, maswali ya ufahamu , insha na maswali ya kutoa ufanano na utofauti wa baadhi ya  dhana katika mada.

      Uwazi wa maswali ya mtihani, maswali yaliyotolewa yana maelekezo wazi na yanaonesha kwa uwazi swali lijibiwe kwa namna ipi , kwani baadhi ya maswali humpa ugumu mwanafunzi, lakini katika mtihani huu  ni bora kwa mwanafunzi wa kidato husika ambapo humwezesha hata kujibu swali vyema, mfano ; sehemu “A”(Alama 10), Ufahamu “Soma kwa umakini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata”. Hii itamrahisishia mwanafunzi kujibu vyema.

Licha ya ubora huo wa mtihani huu, pia mtihani huu wa kidato cha nne (2018), una mapungufu yafutayo;

     Muda wa kuanza na kumaliza mtihani haujabainishwa kama inavyotakiwa, kwa mfano katika mtihani wa Taifa wa Kiswahili kidato cha nne (2018), maelekezo ya muda yana utata kwani katika mtihani huu imeonyeshwa “muda : saa 3:00”, muda huu haujawa wazi kwani hawajaonesha mtihani unaanza saa ngapi  na kumalizika saangapi.  Na pia maelezo hayo yana utata kati ya mtihani unaanza saa tatu kamili au unafanyika kwa masaa matatu.

      Katika mtihani huu sehemu “A” na “B” mgawanyo wa alama haujaoneshwa kulingana na swali mojamoja isipokuwa alama zimewekwa kwa ujumla katika sehemu hizo, pia katika maswali  ya insha  sehemu “C”,”D” na “E” alama zimebainishwa katika swali lakini  katika vipengele vya swali kwa mfano utangulizi, kiini  na hitimisho hawajaonesha idadi ya alama za vipengele hivyo.

     Kutokutolewa  kwa idadi ya maneno katika kuandika kichwa cha ufahamu,Katika mtihani sehemu “A” swali la kwanza kipengele  (d) swali linamtaka  mwanafunzi kuandika kichwa cha habari kinachofaa kwa habari aliyoisoma, lakini hawajatoa au kumwelekeza mwanafunzi ni maneno mangapi anapaswa kuyaandika kwenye kichwa cha habari hicho.

    Mtihani haujazingatia utungaji wa aina mbalimbali za maswali , kwa mfano katika mtihani hakuna maswali ya kuchagua jibu sahihi, maswali ya kuoanisha, pamoja na maswali ya kuandika kweli au si kweli, isipokuwa maswali mengi yaliyo katika mtihani  yanahitaji maelezo zaidi mfano, maswali sehemu  “C” ambayo ni ya insha pamoja na maswali ya sehemu “B”.

     Kutobainishwa kwa idadi ya hoja zinazohitajika katika baadhi ya maswali, kwa mfano swali la (8) hawajabainisha ni hoja ngapi zinahitajika katika  kutofautisha muundo wa barua rasmi na barua za kindugu au kirafiki. Kutokubainisha  idadi ya  hoja zinazohitajika  katika swali husika huweza kupelekea mwanafunzi kuandika hoja nyingi na kusahishiwa hoja baadhi zingine zilizobaki hapewi alama anazostahili au kutokusahishiwa kabisa.

     Hivyo ni muhimu mitihani kutungwa kwa kuzingatia uhalali na uhakika ili kupima kiwango kilichotarajiwa kwa mwanafunzi kwa kipindi fulani cha muda, kwa mfano matumizi ya maneno magumu katika mtihani yatamfanya mwanafunzi asing’amue maswali na hivyo kutojibu  ipasavyo na kupelekea lengo kusudiwa kupotea.

 

 

 

MAREJELEO

Baraza la  mitihani Tanzania (2018). Mtihani wa Kiswahili wa kuhitimu kidato cha nne.Dar-es-salaam:Baraza la mitihani Tanzania

No comments:

Featured Post

 SOMA SIMULIZI ZENYE KUSISIMUA HAPA A. UTAJIRI WENYE UCHUNGU     UTAJIRI WENYE UCHUNGU-1     UTAJIRI WENYE UCHUNGU-2      UTAJIRI WENYE UCH...